Waraka huu nimetumiwa na mwanamuziki mahiri Benno Villa Anthony.................Mkuu, kwanza kabisa namwomba Mwenyezi Mungu akujalie roho ya
uvumilivu ktk kufuatilia taarifa hii. Itakumbukwa kuwa mwanzoni mwa mwaka huu,
nilikuwa na kipindi cha mahojiano na Manju wa muziki na mtangazaji wa TBC,
komredi Masuud Masuud. Kwa vile kipindi kilirudiwarudiwa na huku Manju akitamka
namba yangu ya simu, wengi waliinukuu, na kati ya hao walioinyaka ni Mzee John
Mbulla, aliyekuwa mpiga sax wa Atomic Jazz. Mzee huyu kwa sasa kweli anaumwa
sana. Zaidi ni maradhi ya macho, haoni. Kumbe kwao ni Mpwapwa ila kwa sasa
anahifadhiwa na diwani wa Kibaigwa, Ndugu Richard Kapinye.......0717
303070. Baada ya kusikia kuwa wasanii wanachangiana ili kupata tiba,
Diwani huyo alinipigia na nikazungumza nao wote wawili. Wameniomba nikupe
taarifa hii ili uitoe kwenye vyombo vya habari, ikiwezekana apate msaada wa
tiba. Diwani anasema kuwa John akipata operation ya macho atapona na kuanza
kujitegemea maana nguvu bado anazo. KUMBUKA...Mzee John Mbulla ndiye aliyepiga
Saxaphone kwenye wimbo wa "TANZANIA YETU NDIYO NCHI YA KUSIFIWA",
wakati Mbaraka Mweshehe alipojiunga na Atomic Jazz kwa
muda..............Mkuu Kitime, Nina uhakika kama wana Media wakimtembelea na
kutoa habari zake, naamini wengi wataguswa na kumsaidia. Natanguliza
shukrani zangu za awali. Asante Mkuu.
Kijiwe cha KITIME
Tuesday, May 22, 2012
Monday, May 21, 2012
Robin Gibb wa BeeGees afariki dunia kwa kansa
![]() |
| Marehemu Robin Gibb |
Baada ya kifo cha Donna Summer ( Desemba 31,1948-May 17, 2012), wiki iliyopita,ulimwengu wa muziki umepata pigo jingine baada ya Robin Hugh Gibb, mwanamuziki wa kundi maarufu la BEE GEES kufariki dunia Jumapili 20 May 2012, Robin alizaliwa tarehe 22 Desemba mwaka 1949.
Kundi la Bee Gees lilianzishwa kwa
pamoja na pacha wake Maurice na kaka yao Barry, japo Robin ndie aliyekuwa maarufu zaidi katika kundi hili. Wazazi wao walikuwa Waingereza japo kwa kipindi fulani
walihamia Australia. Inasemekana kundi hili ndilo lililokuwa na mafanikio
kuliko kundi lolote jingine la Pop duniani. Kwa karibu miongo 6 kundi hili
limekuwa jukwaani, likifanya maonyesho. Kundi liliweza kuuza zaidi ya santuri milioni 200.
Watanzania wengi walianza kuwafahamu baada ya kusikia vibao
vyao kama Staying Alive, Night Fever, How deep is your love na kadhalika katika filamu ya filamu ya Saturday
Night Fever.
Tarehe 20 May 2012 Robin
amefariki baada ya matatizo ya muda mrefu ya kansa ya utumbo. Pacha wake
Maurice alifariki kw tatizo hilohilo 2003.
Grammy Awards ambazo kundi hili lilipata:
1977
Best Performance by a Group — "How Deep Is Your Love"
1978 Best Performance by a Group — "Night Fever"
1978 Album of the Year — "Saturday Night Fever"
1978 Producer of the Year — "Saturday Night Fever"
1978 Best Arrangement of Voices — "Stayin' Alive"
2000 Lifetime Achievement Award
2003 Legend Award
1978 Album of the Year — "Saturday Night Fever"
1978 Producer of the Year — "Saturday Night Fever"
1978 Best Arrangement of Voices — "Stayin' Alive"
2000 Lifetime Achievement Award
2003 Legend Award
| Reactions: |
Thursday, May 17, 2012
Donna Summer Hatunae Tena
LaDonna Adrian Gaines aliyejulikana zaidi kwa jina la Donna Summer amefariki leo
Key West Florida akiwa na umri wa miaka 63. Donna Summer amefariki kwa tatizo
la Kansa. Donna alizaliwa tarehe 31 December 1948.
LaDonna alikuwa mmoja wa
watoto saba katika familia yao iliyokuwa inaishi Boston, Marekani. Mwaka 1971
Donna akahamia Austria ambapo alikutana na Helmuth Sommer ambaye walicheza wote
sinema ya Godspell, na wakaoana 1973 walipata mtoto mmoja lakini ndoa ilivunjika
1975. Donna alichukua jina la huyo mumewe aliyekuwa Mjerumani na kulitafsiri
jina kwa Kiingereza na akapata jina la Summer ambalo ndilo lilikuwa jina lake
la jukwaani. Mwaka 1978 wakati anatayarisha kibao cha ‘Heaven Knows’ ndipo
alipokutana na Bruce Sudano na wakaoana July 16, 1980, japo 1979 walipata mtoto
wao kwanza, mtoto wa pili alizaliwa 1981.
Pamoja na nyimbo zake kuigwa
na wanamuziki wengi kama Madonna, Whitney Houston, Diana Ross, Britney Spears, kwa mfano ule wa "Love to Love You Baby" ulikuwa sampled na Beyonce Knowles
na unajulikana kama "Naughty Girl", Donna alikuwa na rundo la awards
na mafanikio mengine, kati ya awards alizopata ni;
- NAACP Image Award
- Juno Award nomination kwa Best Selling International Single,"I Feel Love"
- Multi-Platinum album 3 katika Marekani
- Album zake 11 zilipata Gold nchini Marekani
- Gold singles 12
- American Music Awards 6
- Alikuwa mwanamke wa kwanza Mmarekani mweusi kupata MTV Video Music Awards
- Golden Globe Awards 2
- Donna Summer aliweza kupata jumla ya Grammy Awards 5
- Na aliwahi kuteuliwa mara 12 kwa ajili ya Grammy Award
Alipata heshima nyingine nyingi tu
Tulio cheza muziki wako tutakumiss Donna,
Nakumbuka Love to love you baby, Bad Girls, I feel love na
kadhalika
| Reactions: |
Monday, May 14, 2012
Mjue Issa Juma aliyeimba Sina Makosa
Issa
Juma Singano alikuwa muimbaji, wengi inakuwa rahisi kumfahamu nikisema yule
muimbaji aliyeimba wimbo wa Sina Makosa. Issa alizaliwa Tanga, alianza muziki
akiwa na umri wa miaka 15.Alianza muziki huko kwao Tanga na moja ya vikundi
vingi vilivyokuwepo Tanga wakati ule, na akweza kwenda hadi Uganda ambako alikaa
mpaka 1970 alipoingia Dar es Salaam na akajiunga na Police Jazz ya Dar es
Salaam, miezi sita baadae akahamishiwa Police Jazz ya Tanga. Uwezo wake wa
kuimba ukavuka mpaka hadi Kenya na kusikika na producer maarufu A.P. Chandarana,
huyu akamuita Issa Juma Kericho. April 1971 Issa akahamia Kericho na kujiunga
na Kericho Jazz Band, bendi haikudumu muda mrefu ikasambaratika na Chandarana
akamuajiri Issa kama recording assistant kwenye studio yake maarufu ya Chandarana.
Issa aliishi sana hapa hata kuanza familia yake hapa. Alijaribu kurekodi nyimbo
zake kadhaa lakini hazikupata umaarufu. Mwaka 1977 akaamua kuhamia Nairobi.
Alipofika Nairobi akajiunga na Orchestra Kumbakumba ambayo ilikuwa na
mchanganyiko wa wanamuziki wa Tanzania na Kenya, mmojawapo akiwa mwanamuziki
maarufu muimbaji wa Jamuhuri Jazz band Yusuph Mhando. Mwishoni mwa mwaka 1978
Issa Juma akajiunga na Simba wa Nyika. Kama ilivyohadithia katika makala
zilizopita Issa alifika Simba wa Nyika akaikuta katika mgogoro mkubwa ambapo
wanamuziki wengi walikuwa wakijiandaa kuanzisha Les Wanyika. Nae akawa
mwanamuziki muanzilishi wa Les Wanyika. Na hapa ndipo sauti yake ilikuja
kujulikana sana katika ile album iliyokuwa na nyimbo kama Sina Makosa, Pamela,
Paulina na kadhalika. Aliacha Les Wanyika June 1981 na kwenda kujiunga na Super
Wanyika. Mwaka 1988 alipata ugonjwa wa kupooza na akafariki mwishoni mwa mwaka
1990. MUNGU AMLAZE PEMA PEPONI.
Sunday, April 15, 2012
Abbu Omar Profesa Omar Junior
![]() |
| Ganda la album ya 3 ya Abbu Omar |
Kutokana na kuwa mpiga gitaa maarufu wa Super Volcano Charles Kasembe aliona ni heri kuanzisha bendi aliyoiita Les Volcano. Abbu hakupata nafasi Les Volcano maana ilikuwa imeshajaa wanamuziki. Kasembe alimshauri Abbu awaone Wilson na George Peter ambao wakati huo walikuwa katika jitihada za kufufua tena Simba wa Nyika. Charles mwenyewe alimpeleka Abbu mpaka Bombax Club iliyoko Ngong Road, ambapo ndipo Simba wa Nyika walikuwa wanajiandaa kupiga. Abbu alipandishwa jukwaani siku hiyohiyo na kukabidhiwa gitaa la rhythm, upigaji wake ukampa kazi siku hiyo hiyo. Kwa hiyo pia Abbu akashiriki katika album ya kwanza ya awamu hiyo ambapo album hiyo ilikuwa na nyimbo kama Barua ya Mapenzi, Mama Nirudie, na palikuweko album nyingine na ikafuata album ya tatu iliyokuwa na ule wimbo maarufu wa Shilingi Yaua, Abbu alikaa Simba wa Nyika mpaka 1987 ambapo aliacha bendi, lakini aliendelea kuwa na uhusiano na bendi hiyo na kuendelea kushiriki katika recording mbalimbali za bendi hiyo hadi ya mwisho 1992 kabla ya kifo cha George Peter. Abbu Omar ambaye kwa upigaji wake wa rhythm ulimfanya arith heshima ya Professsor Jnr ikikumbukwa kuwa Professor Omar mkubwa alikuwa ndiye yule aliyeanzisha Les Wanyika. Kwa sasa Abbu Omar yuko Japan ambako ana piga muziki mara nyingine kwa kushirikiana na Fresh Jumbe na Lister Elia
Wednesday, April 11, 2012
Kupukutika kwa Super wa Nyika na kuzaliwa Orchestra Vinavina
Mwishoni mwa mwaka 1981 ndipo Issa juma alipoamua kujitoa Les Wanyika. Sauti yake ilikwishakuwa maarufu kutokana na nyimbo alizoimba akiwa bendi hiyo. Maproducer kutoka kampuni mbalimbali za kurekodi mjini Nairobi waliposikia hilo wakaanza kumfuata ili arekodi katika studio zao. Kampuni iliyoweza kumpata ilikuwa na kampuni ya Meghs iliyokuwa mali ya mhindi mmoja aliyejulikana kwa jina la Babuu. Katika kampuni hiyo alirekodi nyimbo kadhaa zilizokuja pata umaarufu. Kimsingi inaoneka mwanzoni Issa hakuwa na wazo la kuanzisha bendi, mpaka alipolazimika kutafuta jina la bendi ya kuzibeba nyimbo hizo alizorekodi, ndipo kwa mara ya kwanza jina la Super Wanyika lilipozaliwa. Nyimbo zilizotolewa kwa jina la bendi hii zilikuwa kama Anita, Unataka nikupendeje, Jennifer na kadhalika. Wanamuziki walioshiriki katika kazi hizi za mwanzo walikuwa Mohamed Tika, Shoushou Batenga, na Michael Beche waimbaji, huyu Mzee Shoushou alikuwa Mkongo ambaye aliwahi kupitia bendi ya safari Trippers. Mzee Maneno Shaaban alipiga drums, Issa Khalfani Bendera, kwenye solo, Stanley Mtambo gitaa la rhythm, George Madrago gitaa la bezi, Said Makelele na Mambi Iddi wakiwa kwenye trumpet. Nyimbo zilipotoka zilianza kuvuma na kulazimisha bendi ianze kufanya maonyesho. Wanamuziki wakakubaliana na Babuu ambae pamoja na kuwa na studio pia alikuwa na vyombo vya muziki, hivyo akawakodisha vyombo hivyo kwa mkataba maalumu. Super Wanyika ilidumu kwa zaidi ya muda wa miaka mitatu. Baadhi ya wanamuziki waliokuwemo katika kundi hilo ni Mzee Mohamed Tungwa akipiga solo, Abdalah Kimeza kwenye Saxaphone, Jumanne Kilongola kwenye trumpet, Joseph Tito akipiga gitaa la rhythm, Shwaib Ole monduli muimbaji, na wengineo. Lakini bendi hatimae ilikuja kufa kwa makosa yaleyale ya uongozi mbovu. Issa Juma akaanza kusahau kuwapa wanamuziki wenzie haki stahili.
Sauti yake iliendelea kuwa muhimu katika anga la muziki, hivyo akaanza kuingia mikataba tofauti na ule aliyokuwa nao Meghs. Akaingia mkataba na kampuni ya AIT, halafu akaingia mkataba na producer mashuhuri Nairobi wakati huo Bwana Joe Mwangi wa Matunda Production. Sasa kazi ambazo zilifanywa katika mikataba hiyo mipya alitambulisha kuwa zimerekodiwa na bendi aliyoitambulisha kama Wanyika Stars, baadhi ya nyimbo ambazo zilirekodiwa kwa jina hilo ni kama Sigalame,Mpita njia,Bomanga, Mony na kadhalika. Kutokana na wanamuziki hawa walioshiriki kazi hizi, baadhi wakaunda kundi la Sigalame System ambalo halikudumu sana, wengine wakaunda kundi la Orchestra Vinavina, pamoja na kuwa na muziki mzuri hawa Vinavina hawakuwa na bahati ya kupendwa hivyo wakaondoka Nairobi na kuhamia Morogoro Tanzania, wengi wa wanamuziki wa bendi hii asili yao ilikuwa Morogoro,baadae bendi hii ilikuja kuitwa Les Cubano. Les Cubano ilikuwa na wanamuziki kama Michael Beche, Niko Zengekala, Shwaib Ole Monduli, Banza Tax wakiwa ni waimbaji, Mohamed Tungwa na Issa Bendera wapiga solo,Fred Mwalasha rhythm gitaa, George Madrago gitaa la bezi, Mzee Maneno Shaaban akipiga drums, Said Makelele, Mambi Idd, Jumanne Kilongola wapiga trumpet, Kibwana Magati alikuwa anapiga drum na bezi, Abdalaah kimeza na Comson Mkamwa walikuwa wapuliza sax.......itaendeleaaa
Subscribe to:
Posts (Atom)



